Serikali kupitia Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya Nyamagana imesitisha shughuli za ibada nyumbani na katika Kanisa la Mfalme Zumaridi lililopo jijini Mwanza kutokana na kuendeshwa kinyume na taratibu. Uamuzi huo umetangazwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya Nyamagana, Dkt. Philis Nyimbi Novemba 18, 2019.